Powered By Blogger

Translate

Sunday, June 30, 2013

OBAMA AFRIKA KUSINI

tukio ya Afrika

Obama : Igeni mfano wa Mandela

Rais Barack Obama wa Marekani Jumamosi(29.07.2013) amewashajiisha viongozi wa Afrika na duniani kwa jumla kufuata mfano wa rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela kwa kulitanguliza mbele taifa kabla ya nafsi yake.
Obama amesema wakiwa kama viongozi wanashikilia nyadhifa hizo kwa muda na wasidanganyike kiasi cha kufikiri kwamba hatima ya nchi yao haitegemei kadiri watakavyoendelea kuwa madarakani.
Obama alikuwa akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliomjumuisha pia Rais Jacob Zuma mjini Pretoria akiwa katika ziara yake ya wiki moja barani Afrika ambayo tayari imemfikisha Senegal na anatazamiwa kuzuru Tanzania hapo Jumatatu. Obama anafanya ziara hiyo wakati nchi nyingi za Kiafrika zikiwa kwenye mizozo ya kidini, kikabila na mengineyo.
Sio wakati muafaka kuzuru Kenya
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya. Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.
Obama ameamuwa kukwepa kuizuru Kenya kwa sababu ya nchi hiyo kuhusika kwenye mzozo wa kimataifa. Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu imemfungulia mashtaka Rais Uhuru Kenyatta kwa uhalifu dhidi ya ubinaadamu yakiwemo mauaji kuhamisha watu kwa nguvu, ubakaji,ukandamizaji na vitendo vya kinyama vilivyofanywa na wafuasi wake kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 nchini Kenya.
Obama amekaririwa akisema "Wakati sio muafaka akiwa kama rais wa Marekani kuitembelea Kenya wakati masuala hayo yakiwa bado yanafanyiwa kazi na nataraji yatapatiwa ufumbuzi." Amesema tayari ametembelea Kenya mara kadhaa na ataitembelea tena nchi hiyo kipindi cha usoni.
Obama na Zuma walikuwako kwenye Majengo ya Umoja ambako ndiko kuliko ofisi za serikali na ndiko mahala ambapo Mandela alikoapishwa kuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini hapo mwaka 1994 baada ya kuwa gerezani kwa miaka 27 kwa harakati zake za kupambana na utawala wa ubaguzi wa rangi nchini humo.
Rais Barack Obama wa Marekani na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini katika mkutano na waandishi wa habari (29.06.2013). Rais Barack Obama wa Marekani na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini katika mkutano na waandishi wa habari (29.06.2013).
Mandela mwenye umri wa miaka 94 amelazwa katika hospitali mjini Pretoria kwa wiki tatu sasa kutokana na maambukizi ya mapafu. Zuma amewaambia waandishi wa habari hali ya Mandela ni mbaya lakini imara na kwamba taifa zima linamuombea apone.
Obama na mke wake wamekutana na baadhi ya ndugu wa familia ya Mandela lakini kutokana na matakwa yao hakupanga kumuona Mandela ambaye ni mmojawapo wa watu adhimu kabisa duniani.
Obama akimtaja Mandela kwa jina lake la kiukoo amepongeza mjumuiko wa kijamii wa Afrika Kusini kutoka utawala wa kibaguzi na kusema kuwa ni alama inayon'gara duniani.
Mandela shajiisho la dunia
Nelson Mandela alama ya mapambano dhidi ya utawala wa ubaguzi. Nelson Mandela alama ya mapambano dhidi ya utawala wa ubaguzi.
Obama amesema mapambano dhidi ya utawala wa kibaguzi kwa ajili ya uhuru,moyo ya uadilifu wa Madiba kipindi cha nchi cha kihistoria cha taifa hilo kubadilika na kuwa huru na la demokrasia yamekuwa ni mambo yaliomshajiisha yeye mwenyewe binafsi na kuwa kichocheo kwa dunia.
Zuma amemwambia Obama kwamba yeye na Mandela wamefungamanishwa na historia kwa kuwa marais wa kwanza weusi kwa nchi zao na kwa kuwasilisha matumani ya mamilioni ya watu barani na Afrika na wale wanaoishi nje ambao huko nyuma walikuwa wakikandamizwa.
Katika masuala mengine Obama amekataa kujifunga moja kwa moja katika kuunga mkono juhudi za Afrika Kusini kuwania kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.Amesema mfumo wa Umoja wa Mataifa unahitaji kurekebishwa na litakuwa sio jambo la kawaida kulitanuwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa bila kujumuisha uwakilishi wa Afrika.
Uwekezaji wa China haumtishi
Rais Barak Obama katika mkutano na waandishi wa habari Pretoria (29.06.2013). Rais Barak Obama katika mkutano na waandishi wa habari Pretoria (29.06.2013).
Obama pia amesema anataka kuimarisha biashara na Afrika na kuanzisha mazungumzo mapya ya mkataba wa biashara na Afrika ili kuuboresha kwa kampuni za biashara za Marekani.Pia amesema anakaribisha juhudi kubwa zinazofanywa na nchi nyengine kutafuta fursa za biashara barani Afrika ikiwemo China.
Amesema hatishwi na jambo hilo na anafikiri ni zuri ila tu ushauri wake ni kuhakikisha tu kwamba ni kwa ajili ya manufaa ya Afrika kwa kuhakikisha miradi ya uwekezaji ya kigeni inawaajiri Waafrika,haindekezi rushwa au kuchukuwa rasimali zake za asili bila ya kuwafidia Waafrika.
Umuhimu wa Soweto
Kitongoji cha Soweto. Kitongoji cha Soweto.
Obama pia ametowa heshima zake kwa mapambano dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini kwa kutembelea kitongoji cha Soweto ambapo amehutubia wanafunzi katika ukumbi wa jiji wa Chuo Kikuu cha Johannesburg.Takriban vijana 176 wameuwawa katika kitongoji cha Soweto wakati wa maandamano ya vijana dhidi ya marufuku ya utawala wa ubaguzi wa rangi ya kufundisha lugha za kienyeji za Kibantu.Uasi wa Soweto uliimarisha uungaji mkono wa kimataifa dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi na mwezi wa Juni hivi sasa unatambulika kuwa ni Mwezi wa Vijana nchini Afrika Kusini.
Obama atakamilisha ziara yake Afrika Kusini Jumapili ambapo anapanga kutowa hotuba kubwa kuhusu sera ya Marekani kwa Afrika katika Chuo Kikuu cha Cape Town na ataipeleka familia yake katika kisiwa cha Robben kuzuru gereza ambalo Mandela alitumikia miaka 18 ya kifungo chake cha miaka 27 gerezani.

MAPIGANO MAKALI KISMAYO

Wakaazi wa mji wa Kusini wa Somalia Kismayo wanaendela kukikmbia makwao, kutokana na mapigano makali kati ya mababe wa kivita katika eneo hilo.
Takriban raia kumi wameuawa katika mapigano hayo yaliyotokea siku ya Ijumaa.
Mji wa Kismayo ni mji muhimu wa kiuchumi Kusini mwa Somalia na vita hivyo vimechochewa na ushindani mkali wa kithibiti biashara katika mji huo wa bandari.
Ripoti zinasema wapiganaji wa kundi la Ras Kamboni wanaoongozwa na mbabe wa zamani wa kivita aliyejitangaza kuwa rais wa eneo hilo Ahmed Madobe walikabiliana vikali na wapiganaji wa waziri wa zamani wa ulinzi wa Somalia Bare Hirale, ambaye pia anaongoza kundi lingine la waasi katika eneo hilo.
Hali ya Utulivu imeanza kurejea tena mjini humo ambao ni ngome ya zamani ya kundi la kigaidi la Kiislamu la Al Shabaab ambalo lina uhusiano na kundi la Al-Qaeda.
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, Nicholas Kay ametoa wito wa kusitishwa kwa mapigano hayo mara moja, na kutoa wito kwa mababe hao wa kivita kusitisha uhasama kati yao ili kuepusha maafa zaidi ya raia wasiokuwa na hatia.
Wanajeshi wa Kenyan wanaohudumu nchini humo chini ya muungano wa Afrika wanamuunga mkono Bwana Madodbe, lakini serikali ya Somalia halimtambui kama rais na pia haijakubali uamuzi wake wa kutangaza kuwa eneo hilo limejitenga na Somalia.

SUMAYE ATETA NA VIJANA

Dar es Salaam. Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amewatahadharisha vijana kuwa wanaelekea kwenye uchaguzi mkuu wasikubali kupewa rushwa ya kanga, fulana na fedha na mtu yeyote anayetaka kuingia madarakani.
Akizungumza jana alipokuwa kwenye bonanza la michezo la kikundi cha Ukwamani Jogging kilichopo Kawe, alisema vijana wawe makini katika kuchagua mtu mwenye uwezo wa kuongoza ambaye atajali masilahi ya wananchi wake siyo kwa masilahi yake binafsi.
“Najiuliza kama ninajiamini nataka kugombea Kawe au Arusha au Sumbawanga kama ninafaa na wananchi wananiamini mimi ninafaa na wananchi wananihitaji kwa nini niwachochee kwa kanga au fedha ukiona hivyo huyo hawafai kuwaongoza,” alisema na kuongeza:
“Ukiona mtu anatoa kitu ili achaguliwe hafai kuwa kiongozi kwani uongozi ni mzigo,” alisema Sumaye.
Aliwashangaa watu wazima wanaochukua fedha na kuweka mfukoni kisha wanapita mitaani huku wakisema fulani anafaa kwa kuwa anatoa rushwa na fulani hafai kwa kuwa hatoi kitu chochote.
Sumaye alisema anayetoa fedha ili apewe kura huyo hafai kuwa kiongozi kwa sababu atakuwa anawatumikia watu wake waliompa fedha sio mwananchi ambaye alijitolea kumchagua kiongozi hiyo kwa kumpigia kula halali ili aweze kusaidia kumtatulia kero mbalimbali zinazomkabili.
Alisema kama kuna watu wanaumizwa kwa kuambiwa wanapokea au kutoa rushwa huku akiwa anaendelea na kufanya hivyo aache ili asiendelee kuumizwa na hilo.
Sumaye alisema nchi haiwezi kuwa na maendeleo kama viongozi wataendelea kudidimiza nchi kwa rushwa,ufisadi na kuingiza dawa za kulevya nchini.
Alisema viongozi wanaoleta dawa za kulevya kama ni nzuri wangezitumia lakini hawazitumii matokeo yake wanaoathirika ni vijana ambao wanategemewa kulijenga taifa hili.
“Hatuwezi kudidimiza jamii kwa kuwaletea dawa za kulevya ili watoto wa wenzao waharibikiwe kwa nini wasiwape au kutumia hao viongozi ili waathirike wao wenyewe?” alisema Sumaye.

WABUNGE WAINGANGANIA SSERIKALI

Dodoma. Wabunge wa CCM jana waliungana na Kambi Rasmi ya Upinzani kuing’ang’ania Serikali kwa kuupinga Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2013/2014 uliowasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa wakitaka kufanywa mabadiliko mbalimbali ikiwamo kuondoa ongezeko la kodi katika mafuta ya petroli kwa manufaa ya wananchi. Kadhalika, Kamati ya Bajeti imeonyesha kutofautiana na Waziri wa Fedha katika mapendekezo mbalimbali ya muswada huo ikitaka pia kupunguzwa kwa kodi ya mafuta, uagizaji magari huku mwenyekiti wa kamati hiyo akisema kuwa msingi wa mapendekezo yao ni kupunguza gharama za maisha na mfumuko wa bei kwa wananchi. Hata hivyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda jana alipima upepo na kuamua kurudisha kwenye Kamati Muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria za Kodi, na sasa sheria hizo zitapitishwa leo bungeni badala ya jana. Muda mfupi baada ya kuanza kuchangiwa ndani ya Ukumbi wa bunge jana jioni, Makinda alisimama na kuwatangazia wabunge muswaada huo urudishwe tena katika kamati ambako wabunge waliokuwa wametoa mapendekezo ya marekebisho waliungana na Kamati ili kutoa ufafanuzi wa mapendekezo yao. Aidha wabunge hao pamoja na Spika wa Bunge waliusifu na kuunga mkono muswada mbadala uliowasilishwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, uliosomwa na mbunge wa Viti Maalumu Christine Mughwai Lisu kwa niaba ya Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe. Mbali na kuitaka Serikali kuondoa ongezeko la kodi ya mafuta, simu, magari na kupunguza misamaha ya kodi walisema kuwa kitendo cha Serikali kutofuata ushauri wa wabunge kuhusu vyanzo vingine vya mapato, kinawazidishia maisha magumu Watanzania. Mapendekezo hayo ya wabunge, Kamati ya Bajeti na Kambi ya Upinzani yakipita yataweza kumpatia nafuu mwananchi wa kawaida, huku Serikali ikilazimika kujielekeza kwenye vyanzo vingine vya mapato vilivyoainishwa kwenye bajeti, wabunge wakivitaja baadhi kuwa ni pamoja na kodi katika kampuni za madini, kampuni za simu ili kutimiza malengo ya bajeti yake inayofikia Sh18.2 trilioni. Akichangia muswada huo ambao mjadala wake ulihitimishwa jana jioni, kabla ya leo Bunge kukaa kama kamati na kuupitia kifungu kwa kifungu Mbunge wa Mbozi Mashariki Godfrey zambi alisema: “Sikubaliani kabisa na ongezeko lolote la mafuta na dizeli, hayo yanaongeza moja kwa moja ugumu wa maisha kwa Watanzania.” Aliongeza akihoji: Serikali ya CCM ndiyo ipo madarakani, wananchi waliichagua kwa kura nyingi, sasa kwa nini izibe masikio kwa wananchi iliyowachagua? Iwasikilise basi, tuondoe tozo zote katika mafuta.” Kuhusu misamaha ya kodi mbunge huyo alisema kuwa inashangaza kuona kwamba wakati Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CIG) alishauri misamaha ipinguzwe lakini Seikali inaongeza. “Katika misaha ya kodi hapa kuna vimemo vya wakubwa ni vingi, huyu mpe msamaha, Yule mpe msamaha,” alisema Zambi akiwatuhumu baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali kwa kuhusika na mashinikizo ya kusamehe kodi. Mbunge wa Kigoma Mjini (CCM), Peter Serukamba alisema kupandisha tozo katika ndege hakuendani na kasi ya sasa ya Serikali kujenga viwanja vya ndege maeneo mbalimbali nchini. “Hii itasababisha taifa kuwa na ndege mbovu jambo ambalo litasababisha ajali za ndege na kuwaumiza Watanzania.

Saturday, June 29, 2013

TANZANIA NA SRI LANKA KUSHIRIKIANA KIUCHUMI

Dar es Salaam. Tanzania na Sri Lanka zimetiliana saini mikataba ya ushirikiano kwenye maeneo ya uchumi na utalii,huku Rais Jakaya Kikwete akiliombea amani taifa hilo ambalo linakabiliwa na hali mbaya ya kisiasa.
Makubaliano hayo yaliyotiwa saini Ikulu mbele ya marais wote wawili Rais Kikwete na mgeni wake Mahinda Rajapaska yanahusu ushirikiano kwenye eneo la biashara kwa kuanzisha vitega uchumi vitavyowajumuisha wafanyabiashara wa pande zote mbili.
Pia makubaliano hayo yamelenga kuimarisha sekta ya utaliii,ambapo imekubaliwa kuwa kila upande utatumia rasilimali zake kuwavutia watalii na kwamba kwa kuanzia ujumbe wa Tanzania unatazamia kutembelea Sri Lanka baadaye mwaka huu kwa ajili ya kufanya tathimini.
Akizungumzia hatua ya kutiwa saini makubaliano hayo ambayo pia yanahusu eneo la utamaduni, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema nchi zote mbili zinategemea kunufaika hasa kwa kuzingatia kuwa makubaliano hayo yamefanyika kwa kuzingatia historia ya nchi zote.
“ Sasa tumefungua ukurasa mpya.. tunategemea kuona watanzania wakimiminika kwa wingi nchini Sri Lanka kwa ajili ya kutafuta fursa za kibiashara” alisema Membe.
Akizungumza kwenye hafla maalumu ya chakula cha jioni aliyomwandalia mgeni wake, Rais Jakaya Kikwete alipongeza hatua zinazoendelea kuchukuliwa na serikali ya Sri Lanka kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi wake ikiwemo pia kukabiliana na mawimbi mabaya ya kisiasa.
“ Ni matumaini yangu hali ngumu ya kisiasa inayojitokeza sasa itapatiwa ufumbuzi na hatimaye taifa hili litaendelea kuangaza. Naamini mtaendelea kupiga hatua kwenye maeneo ya uchumi na maendeleo kwa ujumla” alisema Rais Kikwete.
Kwa upande wake, Rais wa Sri Lanka Mahinda Rajapaska pamoja na kupongeza ushirikiano wa pande zote mbili lakini pia alielezea matumaini yake kuhusiana na hatua ya ukuzaji uchumi.
Alisema serikali zote zitaendelea kushirikiana kukabiliana na matukio yanayoendelea kutokea duniani ikiwemo pia kukabiliana na vitendo vya ugaidi

Friday, June 28, 2013

CAF YAHAIRISA MAANDAMANO


Dar es Salaaam. Chama cha Wananchi (CUF) kimeahirisha maandamano yaliyopangwa kufanyika Juni 29 mwaka huu kwa sababu Rais Jakaya Kikwete, atakuwa katika Mkutano wa Kimataifa wa Smart Partnership na kushughulikia ziara ya Rais Barack Obama wa Marekani.
Maandamano hayo yalikuwa na lengo la kumfikishia Rais Kikwete ujumbe kuhusu vitendo vya ukatili, wizi, ubakaji na mauaji vinavyofanywa na polisi mkoani Mtwara na kutaka uchunguzi kuhusu matukio ya Arusha.
Hata hivyo kuahirishwa kwa maandamano hayo kunakuja baada ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Suleiman Kova kupiga marufuku maandamano ya aina yoyote na kwamba polisi watapambana na yeyote atakayakaidi amri hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alisema: “Tumepokea barua kutoka Ikulu, kutuomba tusitishe maandamano hayo kwa sababu Rais ambaye ndiye mpokeaji wa maandamano hayo atapokea wageni mbalimbali watakaoingia nchini,” alidai.
Mtatiro alisema barua hiyo ilieleza kuwa haitawezekana Rais kupokea maandamano ya CUF kwa kuwa atakuwa akipokea wageni mbalimbali.
“Sisi tulimwandikia Rais barua kuwa Juni 29 mwaka huu tutakuwa na maandamano ya kuelekea Ikulu,hatukujua kama kutakuwa na ugeni wa marais siku hiyo...tumeahirisha,”alisema

CHADEMA YALIA NA HUJUMA


Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewatuhumu viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Jeshi la Polisi kwa kupanga njama ili kuwaunganisha viongozi wa juu wa Chadema kwenye kesi ya kumwagiwa tindikali, Mussa Tesha.
Viongozi waliotajwa hadharani kuwa wanapanga mbinu hizo ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Mwigulu Nchemba na Ofisa wa Jeshi la Polisi makao makuu, Advocate Nyombi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Uenezi, John Mnyika alisema mikakati hiyo imesababisha kukamatwa kwa Katibu wa Chadema mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kileo wiki iliyopita na kupelekwa Igunga, mkoani Tabora  kuunganishwa kwenye kesi hiyo.
Kileo alikamatwa na kupelekwa makao makuu ya Jeshi la Polisi ambako alihojiwa na jopo la maofisa wa polisi. Kwa mujibu wa Mnyika baada kuhojiwa aliwekwa mahali pasipojulikana na kwamba alizuiwa kuwekewa dhamana.
Mnyika alisema siku iliyofuata, walielezwa kwamba Kileo alipelekwa Igunga kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka akituhumiwa kumwagia tindikali Tesha.
“Tumepata taarifa kwamba Kileo aliteswa vibaya na polisi ili awataje viongozi waliomtuma lakini alikuwa akibishana nao, lakini baadaye aliandikisha mambo waliyoyataka polisi,” alisema.
Akijibu tuhuma hizo, Nchemba alisema hakuna mikakati yoyote inayofanywa kati yake na Nyombi bali hiyo ni hofu yao viongozi wa Chadema kwa sababu wanafahamu kwamba walitenda kitendo hicho.
“Hatuhitaji kikao kudhihirisha hilo kwa sababu ni jambo lililo wazi kwamba Chadema walihusika katika kitendo hicho cha kumwagia tindikali mtu huyo,” alisema.
Kwa upande wake, Nyombi na Msemaji wa Polisi hawakupatikana kuzungumzia suala hilo, lakini Kamanda wa Mkoa wa Tabora, Peter Ouma alisema jeshi hilo litawasaka wahalifu popote walipo na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria bila kujali kama ni wanachama wa vyama fulani au la.
“Mhalifu anaweza pia kuwa mwanachama wa chama fulani kwa hiyo tukimkamata tusihusishwe na mambo ya siasa bali ni kufuata sheria,” alisema kuongeza kuwa Kileo bado hajafikishwa mkoani humo.”
Chadema imeunda jopo la mawakili saba wakiongozwa na Profesa Abdallah Safari na wengine ni Peter Kibatara na Gasper Mwalyela wanaoondoka leo kwenda Igunga wakati Mabere Marando, Tundu Lissu, Nyaronyo Kicheere na Method Kimomogoro watawafuata baadae

NDEGE ZA OBAMA GUNZO


Dar es Salaam. Makachero wa Marekani wameendelea na matayarisho ya mwisho ya ziara ya Rais Barack Obama, ambapo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere walikuwa na kazi ya kuunganisha helikopta za doria.
Makachero hao walikuwa wakiunganisha helikopta sita zilizosafirishwa vipande vipande kutoka Marekani, ambapo meli mbili za kivita na ndege moja pia zimewasili.
Rais Obama tayari yuko katika ardhi ya Afrika, ambapo leo anatarajiwa kwenda Afrika Kusini baada ya kumaliza ziara yake ya kwanza Senegal na anatarajiwa kuwasili nchini Jumatatu.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa jana  unaonyesha Marekani imeleta helikopta hizo kwa ajili ya ulinzi wa Rais Obama, zikiwemo meli zilizobeba helikopta nyingine mbili na ndege.
Habari zilizopatikana kutoka kwa wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,zinasema kuwa helikopta sita zinaunganishwa katika sehemu ya karakana ya Kikosi cha Anga cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Mpashaji mmoja  alisema kuwa helikopta hizo zililetwa kama vipande vipande vilivyosafirishwa kama mzigo kwenye meli za kivita zilizotia nanga jijini Dar es Salaam.
“Nilikaribia kwenye eneo la karakana na nikashangaa kuona jinsi jamaa walivyokuwa ‘bize’ wakiunganisha vyuma mbalimbali na kutengeneza helikopta hizo,” aliongeza mpashaji wetu, ambaye alibahatika kusogelea eneo hilo licha ya kuwepo kwa ulinzi mkali.
Inaaminika kuwa helikopta hizo zitakuwa zinasaidia kusafirisha watu na mizigo kutoka kwenye meli za kivita ambazo zimeegeshwa kwenye Kikosi cha Maji cha JWTZ.
Pia helikopta mbili zinaaminika ziko katika meli ambazo zimeegeshwa huko Kigamboni.
Meli za kivita na ndege ya kijeshi
Katika hatua nyingine, meli mbili za kivita ambazo zimetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu zimeegeshwa Kigamboni.
“Jamaa wana meli kali kwa kweli, mimi nimekuwa askari wa Kikosi cha Maji kwa muda mrefu na kufanya mazoezi na mataifa kadhaa, lakini sijaona meli kama zile

;OBAMA KUPATA PHD




Dar es Salaam. Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT),kimepanga kumtunuku Rais wa Marekani, Barack Obama Shahada ya Heshima ya Uzamivu kwa kutambua mchango wake kwa jamii husasani kwenye maendeleo ya kukuza uchumi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,Makamu Mkuu wa chuo hicho,Profesa Tolly Mbwete alisema tuzo hiyo imethibitishwa na Baraza Kuu la Chuo hicho baadaye kupitishwa na Mkuu wa OUT, Dk Asha Rose Migiro.
“Tumeangalia vigezo vyote muhimu ambavyo mtu anastahili kupewa tuzo kama hii na tukaridhika kuwa Rais huyo anastahili kutunukiwa,” alisema Profesa Mbwete.
Kwa mujibu wa Profesa Mbwete, Rais Obama anakuwa mtu wa tano kutunukiwa tuzo hiyo baada ya kutanguliwa na Mwalimu Julias Nyerere, Rais wa kwanza mweusi wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela, Rais wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Benjamin Mkapa.
Alisema hadi sasa OUT imetoa shahada saba za heshima, ambapo kati ya hizo mbili walitunukiwa mwanataaluma kutoka Marekani, Dk Jane Goodall na Mhadhiri wa Mawasiliano kutoka nchini Uingereza,David Mellor

MISRI APAFAI

Mahasimu wa kisiasa kuandamana Misri 28 Juni, 2013 Wapinzani wa Rais Morsi wanamtaka ajiuzulu wakati wafuasi wake wakimtetea Misri inajiandaa kwa maandamano ya mahasimu wa kisiasa kuhusu Rais Mohammed Morsi , huku maafisa wa usalama nao wakijikita mijini kudhibiti hali ya usalama. Taifa hilo linakumbwa na migawanyiko ya kisiasa na maandamano hayanishi huku pande pinzani zikitaka kuonyesha ubabe wao. Taarifa zinazohusiana Siasa Wafuasi wa Rais Mohammed Morsi wanajiandaa kufanya maandamano ya siku mbili kabla ya maandanao ya upinzani kumtaka rais Mosri kujiuzulu. Wakati huohuo, mtu mmoja aliuawa na wengine kujeruhiwa katika makabiliano Kaskazini Misri Alhamisi jioni. Bwana Morsi kwenye hotuba yake aliyoifanya mwaka mmoja tangu kuwa mamlakani, alisema kuwa maandamano yanatishia uthabiti na demokrasia ya Misri. Majeshi yameamrishwa kushika doria mjini Cairo na katika miji mingine. Bwana Morsi, ambaye ni mwanachama wa chama cha kiisilamu cha Muslim Brotherhood, ni rais wa kwanza wa chama cha kiisilamu kuwahi kuchaguliwa Misri. Mwaka wake wa kwanza mamlakani umekumbwa na ghasia na vurugu pamoja na maandamano ya kila mara huku uchumi nao ukiendelea kudorora. Baadaye leo maelfu ya wafuasi wa Morsi wanatarajiwa kufanya maandamano makubwa kumuunga mkono huku wakipinga matakwa ya upinzani kumtaka ajiuzulu. Baadhi ya makundi ya upinzani pia yanajiandaa kufanya maandamano baadaye mjini Cairo. Muungano rasmi wa upinzani, mnamo Alhamisi ulikataa wito wa rais kufanya mazungumzo nao. Kwenye taarifa yake chama cha National Salvation Front kilisema bado kinajiandaa kuitisha uchaguzi mkuu wa urais.

OBAMA ASIFU SENEGAL

Obama asifu Senegal kwa demokrasia 28 Juni, 2013 - Saa Obama anatarajiwa kwenda Afrika Kusini kisha Tanzania kwa ziara yake ya pili Afrika Rais wa Marekani Barack Obama ambaye yuko katika ziara yake ya Afrika, amesifu nchi ya Senegal kwa kuwa moja ya nchi zenye demokrasia thabiti barani Afrika. Akiwahutubia waandishi wa habari nchini Senegal kwa mkondo wake wa kwanza wa ziara yake Afrika,baada ya mazungumzo na rais Macky Sall, Bwana Obama alisema kuwa Senegal iliandaa uchaguzi huru na wa haki pamoja na kuwa na kipindi salama cha mpito. Taarifa zinazohusiana Siasa, Afrika Pia aliisifu kwa kuwa na mtindo wa kusuluhisha migogoro kwa mazungumzo na mashauriano, wala sio kwa njia ya ghasia. Alisema kuwa Afrika kama bara limepiga hatua kubwa upande wa demokrasia katika miaka ya hivi karibuni. Obama atazuru Afrika Kusini ambako rais mstaafu Nelson Mandela anaugua sana na amelazwa hospitalini. Aliwaambia waandishi wa habari kuwa wanamuombea Mandela pamoja na familia yake. Taarifa zinazohusia

MANDELA BABA WA AFRIKA

Dunia nzima inafuatilia afya ya raisi wa kwanya wa afrika kusini aliye lazwa hospitali kwa zaidi za wiki mbili sasa.Ni wazi kwamba hakuna matumaini ya ku Mandela bado anaugua sana hospitalini Raia wa Afrika kusini wamekesha kwa maombi maombi nje ya makaazi ya zamani ya aliyekuwa rais wa taifa hilo Nelson mtaani Soweto. Rais Jacob Zuma amesema kuwa afya ya shujaa huyo aliyepigana dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini humo inaendelea kuimarika. Taarifa zinazohusiana Afrika Kusini Mandela aliye na umri wa miaka 94 amekuwa hospitalini akiuguwa ugonjwa wa maambukizi ya mapafu. Awali mwanawe wa kike, Makaziwe amesema afya ya babaake inaendelea kuwa njema. Aidha Makaziwe amevikashifu vyombo vya habari kwa kukita kambi nje ya hospitali alikolazwa shujaa huyo akisema wanahabari wanapaswa kumheshimu babaake. Rais Jacob Zuma alisema Alhamisi kuwa hali ya Mandela iliimarika lakini bado yuko hali mahututi. "leo angalau yuko sawa kidogo kuliko nilivyomwacha jana usiku,'' alisema Rais Zuma baada ya kuongea na madakatari wanaomtibu Mandela. Bwana Zuma alifutilia mbali safari yake ya Msumbiji ili kumtembelea Mandela hospitalini. Wakati huohuo mwanawe Mandela Makaziwe alisema Mzee 'bado yupo' na kuwa anaweza kuhisi mtu akimgusa. anae tena.Je nani atamrisi kwa ushujaa wake?